Lima Aafshid
Mshindi wa tuzo ya Ushairi na mwandishi, ambaye mashairi na makala zake zinapinga mila za mfumo dume katika utamaduni wa Afghanistan.
Baada ya kusomea uandishi wa habari, Lima Aafshid amefanya kazi kama ripota wa kujitegemea na mchambuzi wa masuala ya kijamii kwa zaidi ya miaka mitano.
Yeye pia ni mwanachama wa Sher-e-daneshgah, Chama cha washairi cha Chuo Kikuu cha Kabul, ambacho kilitumia mitandao kurusha mashairi yao wakati wa janga kusaidia wanachama wake zaidi ya 200 kudumisha hali ya jamii licha ya janga hilo la kiafya.
*Anguko la Afghanistan ni kama kuzama tena kwenye tope lile lile tulilohangaika nalo kwa miaka ishirini. Nina matumaini, hata hivyo, kwamba tunaweza kuinuka kama tawi, tukifikia nuru kwenye giza la msitu.