Unafahamu nini kuhusu mali ya Afrika iliyoporwa?

Swali 1/6
Nchi: Misri

Jiwe la Rosetta ndio lilikuwa ufunguo wa nyaraka ya jadi Misri. lakini ni nani aliyeligundua jiwe hilo zito (750kg), lililopo sasa katika jumba la ukumbusho Uingereza mnamo 1799?

  • 1. Mvuvi wa Misri
  • 2. Wanaakiolojia Waingereza
  • 3. Wanajeshi wa Ufaransa chini ya utawala wa Napoleon

Jibu sahihi

Historia inayokubalika ni kuwa wanajeshi wa Ufaransa waliligundua jiwe hilo walipochimba msingi wa ngome katika Nile Delta.

Jiwe la Rosetta katika jumba la ukumbusho Uingereza Bloomsbury mnamo Oktoba 14, 2016 London.

Swali 2/6
Nchi: Ethiopia

Vikosi vya Uingereza vilinyakua mali ya Ethiopia katika vita vya Maqdala mnamo 1868. Lakini walitumia ndovu wangapi kubebea mali hiyo?

  • 1. 0
  • 2. 15
  • 3. 3

Jibu sahihi

Ndovu 15 na punda 200 walihitajika kusafirisha mali iliyoporwa Maqdala. Ni pamoja na taji la dhahabu, vikombe na nyaraka za jadi za kikristo ambazo bado zipo katika taasisi tofauti Uingereza.

Taji, lililoundwa Ethiopia takriban 1740, kwa dhahabu, shaba nyekundu na shanga za glasi, rangi na vitambaa zinaonekana katika maonyesho 'Maqdala 1868, kumbukumbu ya uvamizi wa mnamo 1868 na vita vya Maqdala', katika jumba la ukumbusho la Victoria and Albert museum London, mnamo Aprili 5, 2018

Swali 3/6
Nchi: Kenya

Ni wanyama gani wa Tsavo huitwa 'wala mtu' au man-eaters?

  • 1. Maafisa wafisadi Kenya
  • 2. Wanawake wanaoolewa na waume wengi
  • 3. Simba wala watu

Jibu sahihi

Simba wawili wa Tsavo waliwaua wafanyakazi 140 waliokuwa wanajenga reli kutoka Mombasa hadi ziwa Victoria mnamo 1898-1899, kabla ya kupigwa risasi na mhandisi raia wa Uingereza.

Sanamu ya simba wawili kutoka Tsavo waliopo Chicago, Illinois

Swali 4/6
Nchi: Zimbabwe

Mchongo wa mawe wa mwewe wa Zimbabwe ndio nembo kuu ya nchi hiyo. Baada ya kuporwa na wakoloni, kutoka magofu ya mji wa kale. Ni ndege wangapi kati ya wanane waliorudishwa Zimbabwe?

  • 1. 7
  • 2. 0
  • 3. 1

Jibu sahihi

Michongo saba ilikuwepo Zimbabwe kufikia 2003 kipande cha chini cha mchongo mmoja kiliporejeshwa na Ujerumani. Mchongo wa nane upo katika chumba cha kulala cha Cecil Rhodes, ambaye nyumba yake katika mji wa Cape Town Afrika Kusini, sasa ni jumba la ukumbusho.

Swali 5/6
Nchi: Cameroon

Sanamu maarufu la kuchongwa Malkia Bangwa lilichukuliwa kutoka inayojulikana sasa kama Cameroon mwishoni mwa karne ya 19. Wakaazi waliliita sanamu hilo la mwanamke “njuindem”. Maana yake?

  • 1. Mwanamke wa Mungu
  • 2. Shujaa mkubwa
  • 3. Mama mwenye furaha

Jibu sahihi

“Njuindem” inamaanisha “mwanamke wa Mungu” katika lugha ya watu wa Bangwa. Sasa linamilikiwa na wakfu wa Dapper mjini Paris, Ufaransa baada ya Musee Dapper kufungwa mwaka 2017.Bado haijulikani vipi ajenti wa ukoloni wa Ujerumani Gustav Conrau alivyolipata mnamo 1899.

Mchongo wa sanamu la Malkia Bangwa sasa unamilikiwa na taasisi ya Dapper huko Paris, Ufaransa

Swali 6/6
Nchi: Benin

Je shaba za Benin zimetengenezwa kwa nini?

  • 1. Shaba nyeupe
  • 2. Mawe
  • 3. Shaba Nyeusi

Jibu sahihi

Ilioporwa na jeshi la Uingereza 1897, Shaba za Benin zimeundwa kutokana na shaba nyeupe. Nyingi zimesalia katika majumba ya ukumbusho Uingereza, Ujerumani na Marekani.

Mchoro wa shaba nyeupe katika mkusanyiko wa Shaba za Benin

Jifunze zaidi