Mapinduzi yaliyofaulu barani Afrika kwa zaidi ya miongo saba
Takriban mapinduzi 130 yaliyofaulu yametokea katika nchi 36 barani Afrika tangu mwaka 1952 wakati Mfalme Farouk wa Misri alipokuwa rais wa kwanza wa Kiafrika kuondolewa madarakani.
Viongozi waliopinduliwa
-
Rais
Gabon
Soma zaidi... -
Mohamed Bazoum
RaisNiger
Soma zaidi... -
Paul-Henri Sandaogo Damiba
Kaimu RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
Rocha Kabore
RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
Abdalla Hamdok
Waziri MkuuSudan
Soma zaidi... -
Alpha Conde
RaisGuinea
Soma zaidi... -
Bah Ndaw
RaisMali
Soma zaidi... -
Ibrahim Boubacar Keita
RaisMali
Soma zaidi... -
Omar al-Bashir
RaisSudan
Soma zaidi... -
Robert Mugabe
RaisZimbabwe
Soma zaidi... -
Blaise Compaore
RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
Mohamed Mohamed Morsi
RaisMisri
Soma zaidi... -
Francois Bozize Yangouvonda
RaisJamhuri ya Afrika ya Kati
Soma zaidi... -
Amadou Toumani Toure
RaisMali
Soma zaidi... -
Muammar Gaddafi
Kiongozi wa TaifaLibya
Soma zaidi... -
Laurent Gbagbo
RaisIvory Coast
Soma zaidi... -
Hosni Mubarak
RaisMisri
Soma zaidi... -
Zine El Abidine Ben Ali
RaisTunisia
Soma zaidi... -
Mamadou Tandija
RaisNiger
Soma zaidi... -
Kapteni Moussa Dadis Camara
RaisGuinea
Soma zaidi... -
Marc Ravalomanana
RaisMadagascar
Soma zaidi... -
Aboubacar Sompare
RaisGuinea
Soma zaidi ... -
Sidi Ould Cheikh Abdallahi
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Maaouya Ould Sid Ahmed Taya
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Fradique de Menezes
RaisSao Tome and Principe
Soma zaidi... -
Ange-Felix Patasee
RaisJamhuri ya Afrika ya Kati
Soma zaidi... -
Henri Konan Bedie
RaisIvory Coast
Soma zaidi... -
Joao Bernardo Viera
RaisGuinea-Bissau
Soma zaidi... -
Tadjidine Ben Said Massonde
RaisComoro
Soma zaidi... -
Ibrahim Bare Mainassara
RaisNiger
Soma zaidi... -
Johnny Paul Koroma
Kiongozi wa TaifaSierra Leone
Soma zaidi... -
Pascal Lissouba
RaisCongo
Soma zaidi... -
Ahmad Tejan Kabbah
RaisSierra Leone
Soma zaidi... -
Mobutu Sese Seko
RaisDR Congo
Soma zaidi... -
Sylvestre Ntibantunganya
RaisBurundi
Soma zaidi... -
Mohammed Farrah Aidid
RaisSomalia
Soma zaidi... -
Mahamane Ousmane
RaisNiger
Soma zaidi... -
Valentine Strasser
Kiongozi wa TaifaSierra Leone
Soma zaidi ... -
Mohamed Said Djohar
RaisComoro
Soma zaidi... -
Miguel Trovoada
RaisSao Tome and Principe
Soma zaidi... -
Dawda Kairaba Jawara
RaisGambia
Soma zaidi... -
Ernest Shonekan
RaisNigeria
Soma zaidi... -
Joseph Momoh
RaisSierra Leone
Soma zaidi... -
Chadli Bendjedid
RaisAlgeria
Soma zaidi... -
Justin Lekhanya
RaisLesotho
Soma zaidi... -
Moussa Traore
RaisMali
Soma zaidi... -
Mohamed Siad Barre
RaisSomalia
Soma zaidi... -
Hissene Habre Habre
RaisChad
Soma zaidi... -
Samuel Doe
Kiongozi wa TaifaLiberia
Soma zaidi... -
Ahmed Abdallah Abderemane
RaisComoro
Soma zaidi... -
Sadiq al-Mahdi
Waziri MkuuSudan
Soma zaidi... -
Habib Bourguibia
RaisTunisia
Soma zaidi... -
Thomas Sankara
RaisBurkina Faso
Soma zaidi ... -
Jean-Baptiste Bagaza
RaisBurundi
Soma zaidi... -
Tito Lutwa Okello
RaisUganda
Soma zaidi ... -
Leabua Jonathan
Waziri MkuuLesotho
Soma zaidi... -
Muhammadu Buhari
RaisNigeria
Soma zaidi... -
Milton Obote
RaisUganda
Soma zaidi... -
Gaafar Muhammad al-Nimeiry
Kiongozi wa TaifaSudan
Soma zaidi... -
Mohamed Khouna Ould Haidalla
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Louis Lansana Beavogui
Kaimu RaisGuinea
Soma zaidi... -
Shehu Shagari
RaisNigeria
... -
Jean-Baptiste Ouedraogo
RaisBurkina Faso
Soma... -
Saye Zerbo
RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
Goukouni Oueddei
RaisChad
Soma zaidi... -
Hilla Limann
RaisGhana
Soma zaidi... -
David Dacko
RaisJamhuri ya Afrika ya Kati CAR
Soma zaidi... -
Sangoule Lamizana
RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
Luis Cabral
RaisGuinea-Bissau
Soma zaidi... -
Godfrey Binaisa
RaisUganda
Soma zaidi... -
William Tolbert
RaisLiberia
Soma zaidi... -
Mohamed Mahmoud Ould Louly
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Jean-Bedel Bokassa
Rais/MfalmeJamhuri ya Afrika ya Kati CAR
Soma zaidi... -
Fransisco Macias Nguema
RaisEquitorila Guinea
Soma zaidi... -
Yusufu Lule
RaisUganda
Soma zaidi... -
Fred Akuffo
RaisGhana
Soma zaidi... -
Mustapha Ould Salek
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Idi Amin Dada
RaisUganda
Soma tena... -
Joachim Yhombi-Opango
RaisCongo
Soma zaidi... -
Moktar Ould Daddah
RaisMauritania
Soma zaidi... -
Ignatius Kutu Acheampong
Kiongozi wa TaifaGhana
Soma zaidi... -
Ali Soilih
RaisComoro
Soma zaidi... -
Tafari Benti
RaisEthiopia
Soma zaidi... -
James Mancham
RaisSychelles
Soma zaidi... -
Michel Micombero
RaisBurundi
Soma zaidi... -
Ahmed Abdallah Abderemane
RaisComoro
Soma zaidi... -
Yakubu Gowon
RaisNigeria
Soma zaidi... -
Francois Tomalbaye
RaisChad
Soma zaidi... -
Richard Ratsimandrava
Kiongozi wa TaifaMadagascar
Soma zaidi... -
Gabriel Ramanantsoa
RaisMadagascar
Soma zaidi... -
Aman Mikael Andom
Kiongozi wa TaifaEthiopia
Soma zaidi... -
Haile Sellasie I
MfalmeEthiopia
Soma zaidi... -
Hamani Diori
RaisNiger
Soma Zaidi... -
Gregoire Kayibanda
RaisRwanda
Soma zaidi... -
Justin Ahomadegbe Tometin
RaisBenin
Soma zaidi... -
Philibert Tsiranana
RaisMadagascar
Soma zaidi... -
Dkt. Kofi Busia
Waziri MkuuGhana
Soma zaidi... -
Milton Obote
RaisUganda
Soma zaidi... -
Emile Derlin Zinsou
RaisBenin
Soma zaidi... -
Abdirashid Ali Shermarke
RaisSomalia
Soma zaidi... -
Mfalme Idris I
MfalmeLibya
Soma zaidi... -
Ismail al-Azhari
Kiongozi wa TaifaSudan
Soma zaidi... -
Modibo Keita
RaisMali
Soma zaidi... -
Alphonse Massamba-Debat
RaisCongo
Soma zaidi... -
Andrew Juxton-Smith
Kiongozi wa TaifaSierra Leone
Soma zaidi ... -
Christophe Soglo
RaisBenin
Soma zaidi... -
David Lansana
KiongoziSierra Leone
Soma zaidi ... -
Siaka Stevens
Waziri MkuuSierra Leone
Soma zaidi... -
Nicolas Grunitzky
RaisTogo
Soma zaidi... -
Ntare wa 5
MfalmeBurundi
Soma zaidi... -
Leopold Biha
Waziri MkuuBurundi
Soma zaidi... -
Kwame Nkrumah
RaisGhana
Soma zaidi... -
Mfalme Muteza wa pili Wa Buganda
Mfalme/RaisUganda
Soma zaidi... -
Abubakar Tafawa Balewa
Waziri MkuuNigeria
Soma zaidi... -
Maurice Yameogo
RaisBurkina Faso
Soma zaidi... -
David Dacko
RaisJamhuri ya Afrika ya Kati CAR
Soma zaidi... -
Sourou-Migan Apithy
Waziri MkuuBenin
Soma zaidi... -
Moise Tshombe
Waziri MkuuDR Congo
Soma zaidi... -
Ahmed Ben Bella
RaisAlgeria
Soma zaidi... -
Leon M'ba
RaisGabon
Soma zaidi... -
Hubert Maga
RaisBenin
Soma zaidi... -
Fulbert Youlou
RaisCongo
Soma zaidi... -
Sylvanus Olympio
RaisTogo
Soma zaidi... -
Patrice Lumumba
Waziri `MkuuDR Congo
Soma zaidi... -
Abdallah Khalil
Waziri MkuuSudan
Soma zaidi... -
Muhammad VIII al-Amin
MfalmeTunisia
Soma zaidi ... -
Muhammad Naguib
RaisMisri
Soma zaidi... -
Farouk wa Misri
MfalmeMisri
Soma zaidi...
Wimbi Jipya
Afrika imepitia mapinduzi manane yaliyofaulu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Wimbi la sasa la mapinduzi linafuatia kipindi ambapo mapinduzi ya kijeshi yalishuka hadi kiwango cha chini kabisa katika miongo miwili hadi 2020, baada ya kushika kasi katika miaka ya 1970.
Kazi ya kudumu
Baadhi ya viongozi wanaonyakua mamlaka huongoza kwa miongo kadhaa huku wengine wakipinduliwa ndani ya siku chache baada ya kuchukua udhibiti wa serikali.

Rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang Nguema, kwa mfano, amekuwa rais kwa miaka 44 baada ya kutwaa mamlaka mwaka 1979.

Ndiye kiongozi aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi barani Afrika.
Viongozi waliorudi mamlakani baada ya kuondolewa madarakani
Ukanda wa mapinduzi
Nchi nyingi za Sahel zimekuwa na uzoefu wa mapinduzi ya kijeshi. Mapinduzi ya hivi punde katika eneo linalojulikana kama ukanda wa mapinduzi yalitokea Niger na Gabon mwaka 2023.
Viongozi wa kijeshi pia walichukua mamlaka nchini Mali mwaka 2020 na 2021, na katika Chad, Guinea na Sudan mwaka 2021. Burkina Faso ilikumbwa na mapinduzi mawili mwaka wa 2022. Nchi zote hizi, isipokuwa Sudan, ni koloni za zamani za Ufaransa.
Tangu mwaka 2000, robo tatu (19 kati ya 26) ya mapinduzi yaliyofaulu barani Afrika yametokea katika makoloni ya zamani ya Ufaransa. Hii imesababisha baadhi ya watu kuhoji iwapo ushawishi wa Ufaransa barani Afrika una athari ya kuleta misukosuko
Mapinduzi yaliyofanikiwa barani Afrika tangu 1952
Nchi nyingi za Afrika Magharibi na Kati zimekuwa na mapinduzi mengi yenye mafanikio. Takriban nusu ya nchi 17 ambazo zimeathiriwa angalau na mapinduzi manne ziko Afrika Magharibi.
Burkina Faso imekuwa na idadi kubwa zaidi ya mapinduzi yaliyofanikiwa barani Afrika ikiwa na manane, ikifuatiwa na Sierra Leone na Uganda zilizo na saba kila moja.
Ni theluthi moja tu ya nchi za Afrika, nyingi zikiwa za Mashariki na Kusini mwa Afrika, ambazo hazijawahi kuwa na mapinduzi yaliyofanikiwa.
Akiwa na umri wa miaka 34, kufikia 2024, Ibrahim Traoré ndiye rais mwenye umri mdogo zaidi duniani anayehudumu. Alikua kiongozi wa muda wa Burkina Faso kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya Septemba 30, 2022, ambayo yalimwondoa rais wa mpito Paul-Henri Sandaogo Damiba.
Mapinduzi ya kijeshi
Takriban asilimia 90 ya mapinduzi yaliyofaulu yamefanywa na jeshi na kufuatiwa na mamluki kwa asilimia 4. Aina nyingine za mapinduzi barani Afrika ni pamoja na upinzani wa raia, nguvu za kikoloni, vikosi vya waasi na mapinduzi ya ikulu.
Ishi kwa upanga, ufe kwa upanga
Viongozi wengi wanaonyakua madaraka kwa njia ya mapinduzi huondolewa baadaye na wakati mwingine kuuawa.
Mnamo 1972 Jenerali Ignatius Kutu Acheampong aliongoza mapinduzi yasiyo na umwagaji damu kumpindua Waziri Mkuu wa Ghana aliyechaguliwa kidemokrasia Dk Kofi Busia. Miaka sita baadaye, alitimuliwa katika mapinduzi ya ikulu na kuuawa kwa kufyatuliwa risasi mwaka mmoja baadaye.
Thomas Sankara alikua rais wa Burkina Faso mwaka 1983 kufuatia mapinduzi kwa niaba yake alipokuwa chini ya kifungo cha nyumbani. Tarehe 15 Oktoba 1987, Sankara aliuawa na kundi lenye silaha wakati wa mapinduzi yaliyoongozwa na mrithi wake Blaise Compaoré.
Gaafar Nimeiry alimuondoa madarakani Mkuu wa Jimbo la Sudan Ismail al-Azhari mwaka 1969 na kuchukua madaraka, kwanza kama mkuu wa utawala wa kijeshi, kisha kama rais kabla ya kupinduliwa mwaka 1985.
Jean-Baptiste Bagaza alimuondoa Rais wa Burundi Michel Micombero mwaka 1976 na kuchukua mamlaka. Miaka kumi na moja baadaye alifukuzwa, na kulazimika kwenda uhamishoni.
Omar al-Bashir aliingia madarakani mwaka 1989 wakati, akiwa Brigedia Jenerali katika Jeshi la Sudan, aliongoza kundi la maafisa katika mapinduzi ya kijeshi ambayo yaliiondoa madarakani serikali iliyochaguliwa kidemokrasia. Aliendelea kuhudumu kama mkuu wa nchi ya Sudan chini ya vyeo mbalimbali kuanzia 1989 hadi 2019, alipoondolewa madarakani kwa mapinduzi.
François Bozizé Yangouvonda alichukua mamlaka mwaka 2003 na kuwa rais wa sita wa Jamhuri ya Afrika ya Kati. Alipinduliwa miaka 10 baadaye.
Kuiweka katika familia
Kunyakua madaraka ni mila ya familia katika baadhi ya nchi. Rais wa Guinea ya Ikweta Francisco Macías Nguema alipinduliwa na mpwa wake, Teodoro Obiang Nguema Mbasogo, katika mapinduzi ya umwagaji damu mwaka 1979. Teodoro alimrithi. Kufikia 2024, ndiye kiongozi wa sasa wa kitaifa asiye wa kifalme duniani kuongoza kwa muda mrefu zaidi duniani.
Laurent Kabila alimpindua Rais Mobutu Sese Seko mwaka 1997 na kuwa rais wa tatu wa DR Congo. Alirithiwa na mwanawe Joseph Kabila aliyekuwa na umri wa miaka 29 wakati huo baada ya kuuawa na mmoja wa walinzi wake.