Chemsha bongo: Mtanzania anayejijengea kaburi linalotarajia kugharimu takriban dola 500,000 hufanya kazi ya aina gani?

Swali 1/7

image

Mtanzania anayejijengea kaburi linalotarajia kugharimu takriban dola 500,000 hufanya kazi ya aina gani?

1. Daktari wa upasuaji wa ubongo
2. Daktari wa tiba ya kiasili
3. Muuzaji dhahabu



Swali 2/7

image

Ni lengo gani kuu la Mwanamfalme William wa Uingereza kuzuru Afrika?

1. Kukabiliana na ujangili na uhifadhi wa wanyama
2. Kuimarisha uhusiano wa Uingereza na bara Afrika.
3. Kuimarisha sekta ya utalii barani Afrika.



Swali 3/7

image

Ni mchezaji gani wa hivi karibuni aliyeorodheshwa kuwa miongoni mwa wachezaji ambao wamefunga mabao 500 na zaidi?

1. Neymar
2. Lionel Messi
3. Zlatan Ibrahimovic



Swali 4/7

image

Bilionea wa Japan anatarajia kuelekea mwezini pamoja na kundi la wasanii mwaka gani?

1. Kufikia 2020
2. Kufikia 2023
Kufikia 2030



Swali 5/7

image

Bingwa wa Olimpiki Eliud Kipchoge alitumia muda gani kukamilisha mbio za Marathon zilizofanyika Berlin.

1. Saa 2 Dakika 2 Sekunde 57
2. Saa 2 Dakika 1 Sekunde 30
3. Saa 2, Dakika 1 na Sekunde 39



Swali 6/7

image

Ni kitu gani ambacho kilizua gumzo wakati mwanamuziki wa Uganda Bobi Wine alipokuwa akirudi nchini Uganda?

1. Begi
2. Mkongojo
3. Suti



Swali 7/7

image

Ni nchi gani ambayo imehalalisha matumizi ya bangi kwa watu wazima wiki hii barani Afrika?

1. Mali
2. Afrika Kusini
3. Ghana




1. Mtanzania anayejijengea kaburi linalotarajia kugharimu takriban dola 500,000 hufanya kazi ya aina gani?

Sahihi: Daktari wa tiba ya kiasili

Dkt Anthony Mwandulami ni daktari wa tiba ya kiasili na lengo lake ni kuihifadhi historia yake baada ya kifo.
Mwandulami anasema ndani ya kaburi hili, atazikwa yeye pamoja na wake zake watatu.
Amechimba chini mita 12 na amesema mwili wake utakaushwa kabla ya kuhifadhiwa.
https://www.bbc.com/swahili/habari-45584179



2. Ni lengo gani kuu la Mwanamfalme William wa Uingereza kuzuru Afrika?

Sahihi: Kukabiliana na ujangili na uhifadhi wa wanyama

Mwanamfalme William wa Uingereza ataruzu Afrika kwa lengo la kukabiliana na ujangili na uhifadhi wa wanyama.
William ni rais wa mashirika yanayotetea uhifadhi wa wanyama ya United for Wildlife na Tusk Trust.
Anatarajiwa kuzuru Tanzania, Kenya na Namibia.
Usikose kupata habari za mwanamfalme Harry kwenye



3. Ni mchezaji gani wa hivi karibuni aliyeorodheshwa kuwa miongoni mwa wachezaji ambao wamefunga mabao 500 na zaidi?

Sahihi: Zlatan Ibrahimovic

Mshambuliaji wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic, amejiunga na wachezaji ambao wamefunga magoli 500 na zaidi wakichezea timu kubwa ya klabu na taifa.
Ibrahimovic, alifunga bao la kushangaza dhidi ya Toronto nchini Marekani.
Messi tayari ni miongoni mwa wachezaji ambao wamefunga magoli 500 kwa hivi sasa amefunga magoli 365 katika mechi zote.



4. Bilionea wa Japan anatarajia kuelekea mwezini pamoja na kundi la wasanii mwaka gani?

Sahihi: Kufikia 2023

Bilionea wa Kijapani Yusaku Maezawa,42, anatarajiwa kusafiri mwezi kufikia mwaka 2023 pamoja na kundi la wasanii.
Maezawa,hajafahamu bado ni kiasi gani cha fedha anapaswa kukilipa kwa safari hiyo ambayo itawaunganisha pamoja na mabilionea wengine wawili ambao hawajulikani sana duniani.
Mjapani huyo alianza kama mjasiriamali wa kuuza CD ambazo zilikuwa adimu.



5. Bingwa wa Olimpiki Eliud Kipchoge alitumia muda gani kukamilisha mbio za Marathon zilizofanyika Berlin.

Sahihi: Saa 2, Dakika 1 na Sekunde 39

Bingwa wa Olimpiki Eliud Kipchoge alitumia muda wa saa 2 dakika 1 na sekunde 39.
Kipchoge, mwenye umri wa miaka 33, ameshinda mara kumi kati ya marathon 11 alizokimbia.
Kipchoge kwa sasa ndiye anayeshikilia rekodi mpya ya mbio za marathon duniani.



6. Ni kitu gani ambacho kilizua gumzo wakati mwanamuziki wa Uganda Bobi Wine alipokuwa akirudi nchini Uganda?

Sahihi: Begi

Bobi alipowasili Uganda kutoka Marekani, alikokuwa amekwenda kupokea matibabu alikuwa na begi nembo ya bidhaa za kifahari - Luis Vuitton.
Alikuwa na mkongojo lakini haukuzua mjadala miongoni mwa wakosoaji wake.
https://www.bbc.com/swahili/habari-45588883



7. Ni nchi gani ambayo imehalalisha matumizi ya bangi kwa watu wazima wiki hii barani Afrika?

Sahihi: Afrika kusini

Afrika kusini
Mahakama ya Kikatiba nchini Afrika Kusini imehalalisha utumiaji wa bangi kwa watu wazima katika maeneo faragha.
Mwezi Aprili Zimbabwe ilikuwa nchi ya pili barani Afrika baada ya Lesotho kuhalalisha bangi kwa matumizi ya kiafya.
https://www.bbc.com/swahili/habari-45570162