Olimpiki Tokyo 2020: Wanariadha wa Afrika wanaoangaziwa kufanya vyema

  • Taoufik Makhloufi, 33

    Algeria Mwanariadha

    Taoufik Makhloufi ni mwanariadha anayekimbia mbio za masafa ya kati (mita 800 na mita 1,500).

    Alishiriki kwa mara ya kwanza katika michuano ya Olimpiki ya London 2012 na kushinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 1,500 na medali za shaba mbili katika michuano ya Olimpiki ya Rio ya mwaka 2016.

  • Wali Bidani, 27

    Algeria Mnyanyua chuma

    Wali Bidani ni mnyanyua chuma kutoka Algeria ambaye alichomoza katika michuano ya Olimpiki ya 2012 ya London na kisha kushiriki pia Rio mwaka 2016.

  • Azenaide Carlos, 31

    Angola Mpira wa mikono

    Azenaide Carlos ni mchezaji wa mpira wa mikono na yumo kwenye timu ya taifa ya wanawake ya Angola.

    Ameshiriki michuano mitatu ya Olimpiki tangu mwaka 2008.

  • Nijel Amos, 27

    Botswana Mkimbiaji

    Nijel Amos ni mwanariadha kutoka Botswana na mshindi wa medali ya fedha wa mbio za 800m wanaume katika michuano ya Olimpiki ya London ya mwaka 2012.

    Michuano ya Tokyo 2020 itakuwa ni Olimpiki a tatu kwake.

  • Hugues Fabrice, 28

    Burkina Faso Mrukaji

    Hugues Fabrice ni mwanariadha wa Burkina Faso anayecheza mchezo wa miruko mitatu ambaye alinyakua medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya riadha ya mwaka 2019

  • Francine Niyonsaba, 28

    Burundi Mwanariadha

    Francine Niyonsaba ni mwanariadha wa Burundi ambaye alishinda medali ya fedha katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016 na michuano ya dunia ya riadha ya mwaka 2017 katika upande wa mbio za mita 800.

  • Cheick Cisse, 27

    Côte D’Ivoire Taekwondo

    Cheik Cisse aliweka historia kwa kushinda medali ya kwanza kabisa ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016.

    Alikuwa pia mwafrika wa kwanza kushinda medali ya dhahabu ya Taekwondo.

  • Marie-Josée Ta Lou, 32

    Côte D’Ivoire Mwanariadha

    Marie-Josée Ta Lou ni mkimbiaji wa mbio fupi za mita 100 na 200.

    Ni mshindi wa medali ya shaba kwa wanawake katika mashindano ya riadha ya dunia ya mwaka 2019 na alishika nafasi ya nne katika michuano ya Olimpiki ya Rio 2016 katika mbio za 100m na 200m.

  • Haydy Morsy, 22

    Misri Michezo mchanganyiko

    Haydy Morsy ni mwanamichezo wa kisasa ambaye anashiriki michezo tofauti mitano lakini akitilia mkazo zaidi kuogelea na mbio za farasi.

    Tokyo 2020 ni michuano yake ya pili ya Olimpiki.

  • Azmy Mehelba, 30

    Misri Mlenga shabaha

    Azmy Mehelba ni mlenga shabaha wa Misri ambaye michuano ya Tokyo ni Olimpiki yake ya tatu.

    Ameshinda medali ya dhahabu hivi karibuni katika michuano ya Kombe la Dunia ya ISSF Mei, 2021.

  • Giana Farouk, 26

    Misri Karate

    Giana Farouk ni mcheza karate kutoka Misri ambaye anashiriki michuano ya Olimpiki kwa mara ya kwanza.

    Alishinda medali ya dhahabu mwaka 2016 na fedha mwaka 2018 katika michuano ya karate ya dunia.

  • Merhawi Kudus, 27

    Eritrea Mwendesha baiskeli

    Merhawi Kudus, 27 ni mwendesha baiskeli kutoka Eritrea ambaye alishika nafasi ya tatu katika mashindano ya Uturuki ya mwaka 2019.

    Alishika nafasi ya kwanza na ya pili katika vipengele vya binafsi na jumla kwenye mashindano ya Eritrea ya 2021. Anashiriki Olimpiki kwa mara ya kwanza.

  • Amanuel Gebreigzabhier

    Eritrea Mwendesha baiskeli

    Amanuel Gebreigzabhier anashiriki Olimpiki kwa mara ya kwanza. Amanuel aliibuka mshindi wa mashindano ya Afrika ya baiskeli ya mwaka 2018.

  • Mosana Debesay, 27

    Eritrea Mwendesha baiskeli

    Mosana Debesay ni mwendesha baiskeli kutoka Eritrea ambae alishinda mashindano ya wanawake ya Afrika ya mwaka 2018 na 2019.

    Ni ndugu wa mwendesha baiskeli mwengine wa Eritrea Mekseb Debesay.

  • Letesenbet Gidey, 23

    Ethiopia Mwanariadha

    Letesenbet Gidey ni mkimbiaji wa mbio ndefu kutoka Ethiopia ambaye anashikilia rekodi ya dunia ya mbio za mita 5,000 na hivi karibuni amevunja rekodi ya mita 10,000.

    Alishinda medali ya shaba katika mashindano ya riadha ya dunia katika mbio za mita 10,000 mwaka 2019.

  • Selemon Barega, 21

    Ethiopia Mwanariadha wa masafa marefu

    Selemon Barega ni mkimbiaji wa mbio ndefu kutoka Ethiopia ambaye alishinda medali ya fedha katika michuano ya riadha ya dunia kwenye mbio za mita 5,000 mwaka 2019.

    Michuano ya Tokyo 2020 itakuwa ndiyo olimpiki yake ya kwanza.

  • Yomif Kejelcha, 23

    Ethiopia Mwanariadha wa mbio za masafa marefu

    Yomif Kejelcha ni mwanariadha wa Ethiopia ambaye Tokyo 2020 itakuwa ni michuano yake ya awali ya Olimpiki.

    Kejelcha ameshinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 3,000 kwenye mashindano ya dunia ya ndani ya mwaka 2018.

    Pia alishinda medali ya fedha katika mbio za 10,000m kwenye mashindano ya dunia ya riadha ya mwaka 2019.

  • Lelisa Desisa, 31

    Ethiopia Mwanariadha

    Lelisa Desisa ni mkimbiaji wa mbio ndefu wa Ethiopia na mshindi wa medali ya dhahabu ya mbio za marathoni katika mashindano ya riadha ya dunia ya mwaka 2019.

  • Shura Kitata, 25

    Ethiopia Mwanariadha

    Shura Kitata ni mwanariadha kutoka Ethiopia nayekimbia mbio ndefu.

    Alishinda medali ya dhahabu katika michuano ya marathoni ya London mwaka 2020 na kumshinda gwii kutoka Kenya Eliud Kipchoge. Kitata alishika nafasi ya pili katika mbio hizo mwaka 2018 ambapo mshindi alikuwa Kipchoge.

  • Gudaf Tsegay, 24

    Ethiopia Mwanariadha

    Gudaf Tsegay ni mwanariadha wa Ethiopia anayekimbia mbio za masafa ya kati ambaye alivunja rekodi ya michuano ya ndani ya mbio za mita 1,500 huko Liévin, Ufaransa Februari 2021.

    Alishinda medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya riadha ya mwaka 2019.

  • Gina Bass, 26

    Gambia Mwanariadha

    Gina Bass ni mkimbiaji wa mbio fupi kutoka Gambia ambaye katika mashindano ya Afrika 2019 alishinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 200 wanawake.

    Michuano ya Tokyo 2020 itakuwa ni olimpiki yake ya pili.

  • Julius Yego, 32

    Kenya Mtupa mkuki

    Julius Yego ni mtupa mkuki kutoka Kenya ambaye alishinda medali ya fedha katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016.

    Anafahamika kwa jina la utani la Mr Youtube kwa kuwa alinoa kipaji chake katika mchezo huo kwa kutazama video kupitia mtandao wa kijamii wa YouTube.

  • Brigid Kosgei, 27

    Kenya Mwanariadha

    Brigid Kosgei ni mkimbiaji wa mbio ndefu kutoka Kenya ambaye ni mshindi wa mbio za marathoni za Chicago mwaka 2018 na 2019 na pia mshindi wa mbio za marathoni za London mwaka 2019 na 2020.

    Kosgei anashikilia rekodi ya dunia kwa wanawake ya marathoni ya 2:14:04 ambayo aliiweka katika michuano ya marathoni ya Chicago ya 2019. Mashindano ya Tokyo yatakuwa Olimpiki yake ya kwanza.

  • Eliud Kipchoge, 36

    Kenya Mwanariadha

    Eliud Kipchoge ni mwanariadha nyota wa mbio ndefu kutoka kenya.

    Gwiji huyu anashikilia rekodi ya dunia ya mbio za marathoni ya 2:01:39 ambayo aliiweka Septemba 16, 2018 katika michuano ya marathoni ya Berlin ya mwaka 2018.

    Alishinda medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016.

  • Beatrice Chepkoech, 29

    Kenya Mwanariadha

    Beatrice Chepkoech anashikili rekodi ya dunia ya mbio za kuruka viunzi.

    Mwanariadha huyo kutoka Kenya ni mshindi wa medali ya dhahabu kwa mbio za mita 3,000 kuruka viunzi katika mashindano ya dunia ya mwaka 2019.

  • Faith Kipyegon, 27

    Kenya Mwanariadha

    Faith Kipyogen ni mkimbiaji wa mbio ndefu kutoka Kenya ambaye alishinda medali ya dhahabu ya mita 1,500 katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016.

    Alishinda pia medali yafedha katika mashindano ya dunia 2017 na medali nyengine ya fedha 2019 katika mashindano ya dunia ya riadha.

  • Khadija Mardi, 30

    Morocco Ndondi

    Khadija Mardi ni bondia kutoka Morocco. Alishiriki Olimpiki ya 2016 jiini Rio lakini alitolewa kwenye mechi ya pili ya robo fainali ya wanawake ya uzani wa kati (69-75kgs).

    Alishinda medali ya shaba katika michuano ya dunia ya masumbwi ya mwaka 2019.

  • Rababe Arafi, 30

    Morocco Mwanariadha

    Rababe Arafi ni mwanariadha kutoka Morocco ambaye alishinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 1,500 wanawake kwenye michuano ya Ligi ya Almasi ya IAAF mwaka 2019.

    Michuano ya Tokyo 2020 itakuwa ni olimpiki yake ya pili.

  • Ramzi Boukhiam, 27

    Morocco Mteleza mawimbi

    Ramzi Boukhiam ni mchezaji wa kulipwa wa kuteleza mawimbi ya bahari kwa ubao.

    Michuano ya Tokyo ya 2020 itakuwa ni mashindano yake ya kwanza ya Olimpiki. Pia anakuwa ni mteleza mawimbi wa kwanza kuiwakilisha Morocco katika michuano ya Olimpiki.

  • Soufiane El Bakkali, 27

    Morocco Mwanariadha

    Soufiane El Bakkali ni mshindi wa medali ya fedha wa mbio za kuruka viunzi katika michuano ya dunia ya riadha ya IAAF ya mwaka 2017.

    Michuano ya Rio 2016 ilikuwa ni Olimpiki yake ya kwanza.

  • Maria Machava,

    Msumbiji Mwendesha mashua

    Maria Machava ni mwendesha mashua wa Msumbiji ambaye atashiriki michuano ya olimpiki kwa mara ya kwanza Tokyo.

  • Deisy Nhaquile

    Msumbiji Mwendesha mashua

    Deisy Nhaquile ni mwendesha mashua wa Msumbiji ambaye atashiriki michuano ya olimpiki kwa mara ya kwanza.

    Alikuwa ni mshindi wa michuano ya Afrika mwaka 2019 kwa mashua aina ya 420.

  • Denise Parruque

    Msumbiji Uendesha mashua

    Denise Parruque ni mwendesha mashua wa Msumbiji ambaye atashiriki michuano ya olimpiki kwa mara ya kwanza jijini Tokyo.

    Akiwa na mwendesha mashua mwenzake Maria, alishinda michuano ya Afrika ya mwaka 2019.

  • Maike Diekmann, 27

    Namibia Mpiga makasia

    Maike Diekmann ni mwendesha mtumbi ambaye ataiwakilisha Namibia kwenye michuano ya Olimpiki kwa mara ya kwanza kupitia mchezo wa kuendesha mtumbwi.

  • Beatrice Masilingi, 18

    Namibia Mwanariadha

    Beatrice Masilingi ni mkimbiaji wa mbio fupi za mita 400 kutoka Namibia ambaye anarekodi ya kasi ya tatu ya vijana wa miaka chini ya 20.

    Hata hivyo hataruhusiwa kushiriki mbio za mita 400 katika michuano ya olimpiki kwa kuwa na kiwango kikubwa cha homoni za kiume za testosterone, lakini ataruhusiwa kushiriki mbio nyengine.

  • Christine Mboma, 18

    Namibia Mwanariadha

    Christian Mboma ni mkimbiaji wa mbio fupi kutoka Namibia ambaye amevunja rekodi ya mita 400 kwa wakimbiaji wenye umri chini ya miaka 20 mwaka 2021.

    Hata hivyo hataruhusiwa kushiriki mbio za mita 400 katika michuano ya olimpiki kwa kuwa na kiwango cha juu cha homoni za kiume za testosterone, lakini ataruhusiwa kushiriki mbio nyengine.

  • Aminatou Seyni, 24

    Niger Mwanariadha

    Aminatou Seyni ni mwanariadha kutoka Niger ambaye alishiriki michuano ya dunia ya ya mwaka 2019.

  • Blessing Okagbare, 33

    Nigeria Mwanariadha

    Blessing Okagbare ni mwanariadha anayekimbia mbio fupi kutoka Nigeria.

    Anashikilia rekodi ya mbio za mita 100 ya michuano ya Jumuiya ya Madola ya sekunde 10.75, lakini aliivunja rekodi hiyo katika mashindano ya kufuzu olimpiki ambapo aliandikisha muda wa sekunde 10.63 mwezi Juni 2021.

    Rekodi hiyo sasa ndiyo kubwa zaidi barani Afrika na inafungana na ile iliyowekwa na mwanariadha wa Jamaica Shelly-Ann Fraser-Pryce mwaka 2021 pia.

  • Elizabeth Anyanacho, 22

    Nigeria Taekwondo

    Elizabeth Anyancho ni mwanamke wa pili na wa pili kutoka Nigeria kufuzu kushiriki michuano ya Olimpiki katika mchezo wa Taekwondo. Mara ya mwisho mwanamke kutoka Nigeria kushiriki Olimpiki kupitia Taekwondo ilikuwa miaka 16 iliyopita.

  • Divine Oduduru, 24

    Nigeria Mwanariadha

    Divine Oduduru alishiriki olimpiki kwa mara ya kwanza jiini Rio mwaka 2016.

    Mwanariadha huyo alikuwa mkimbiaji wa mbio fupi pekee kwa upande wa wanaume kutoka Nigeria kufikia hatua ya nusu fainali.

  • Tobi Amusan, 24

    Nigeria Mwanariadha

    Tobi Amusan mwanariadha anayeshiriki mbio fupi za kawaida na kuruka viunzi. Ni mshindi wa dhahabu katika mbio za mita 100 kuruka viunzi kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola 2018 yaliyofanyika Australia.

    Alishiriki kwa mara ya kwanza michuano ya olimpiki Rio 2016 lakini aliishia nusu fainali.

  • Ese Brume, 25

    Nigeria Mwanariadha

    Ese Brume ni moja kati ya wanariadha wa kike watatu kutoka Afrika ambao wameruka umbali wa mita saba ama zaidi.

    Alishiriki michuano ya Olimpiki kwa mara ya kwanza Rio 2016 ambapo alimaliza katika nafasi ya tano.

    Alishinda medali ya shaba katika michuano ya riadha ya dunia mwaka 2019.

  • Chukwuebuka Enekwechi, 28

    Nigeria Urushaji tufe

    Chukwuebuka Enekwechi ni mrusha tufe ambaye alishinda medali ya fedha katika michuano ya Jumuiya ya Madola ya mwaka 2018.

    Pia alishika nafasi ya nane katika mashindano ya dunia ya mwaka 2019.

  • Usheoritse Itsekiri, 23

    Nigeria Mwanariadha

    Usheoritse Itsekiri ni mwanariadha anayekimbia mbio fupi na mshindi wa medali ya shaba ya michuano ya Afrika.

  • Esther Toko, 21

    Nigeria Mpiga makasia

    Esther Toko ni mpiga makasia katika mbio za mitumbwi ambaye ambaye alishinda medali za shaba na fedha katika mashindano ya Ufukweni ya Afrika yaliyofanyika visiwani Cape Verde 2019.

    Michuano ya Tokyo 2020 itakuwa ni olimpiki ya kwanza kwa Toko kushiriki.

  • Ayomide Emmanuel Bello, 19

    Nigeria Mpiga makasia

    Ayomide Emmanuel Bello ni mpiga makasia wa mbio za haraka na maporomoko kutumia mtumbwi. Anakuwa mwanamke wa kwanza kuiwakilisha Nigeria katika michuano ya Olimpiki kupitia mchezo huo.

    Bello ni mshindi wa medali nne za dhahabu katika mashindano ya Afrika ya mwaka 2019 katika vipengele vya C-1 200m, C-1 500m, C-2 200m na C2 500m

  • Rodney Govinden, 35

    Ushelisheli Uendesha Mashua

    Rodney Govinden ataiwakilisha nchi ya visiwa vya Ushelisheli katika michuano ya Olimpiki ya Tokyo 2020.

    Hii ni olimpiki yake ya pili baada ya kushiriki kwa mara ya kwanza Rio 2016.

  • Wayde Van Nierkerk, 29

    Afrika Kusini Mwanariadha

    Wayde Van Nierkerk ni mwanariadha anayekimbia mbio fupi kutoka Afrika Kusini amabye alishinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 400 katika michuano ya Olimpiki ya Rio 2016.

    Anashikilia rekodi ya dunia ya sekunde 43.03 akivunja rekodi ambayo iliwekwa na gwiji wa zamani wa Marekani Michael Johnson.

  • Chad Le Clos, 29

    Afrika Kusini Uogeleaji

    Chad le Clos ni mwogeleaji kutoka Afrika Kusini ambaye ameshinda medali mbalimbali ikiwemo ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki ya London 2012 na fedha mbili Rio 2016.

  • Akani Simbine, 27

    Afrika Kusini Mwanariadha

    Akani Simbine ni mwanariadha anayekimbia mbio fupi kutoka Afrika Kusini ambaye alishinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 100 kwenye michuano ya nchi za Jumuiya ya Madola.

    Alishika nafasi ya nne katika mashindano ya dunia ya mwaka 2019.

  • Caitlin Rooskrantz, 19

    Afrika Kusini Sarakasi

    Caitlin Rooskrantz atashiriki michuano ya olimpiki kwa mara ya kwanza Tokyo.

    Alishinda mashindano ya sarakasi ya Afrika 2018 na ya dunia 2019.

    Tokyo 2020 itakuwa ndio michuano yake ya kwanza ya olimpiki.

  • Erin Sterkenburg, 18

    Afrika Kusini Kupanda vihunzi

    Erin Sterkenburg ni mpanda vihunzi pekee kutoka Afrika Kusini ambaye ataliwakilisha bara la Afrika katika mchezo huo kwenye michuano ya Olimpiki ya Tokyo 2020.

    Ni mshindi wa michuano ya IFSC Afrika ya mwaka 2020.

  • Henri Schoeman, 29

    Afrika Kusini Mwanariadha

    Henri Schoeman ni mwanaraidha wa Afrika Kusini anayeshindana katika michezo mchanganyiko mitatu, Triathlon (kukimbia, kuendesha baiskeli na kuogelea). Ni mshindi wa medali ya dhahabu wa michuano ya Jumuiya ya Madola 2018.

    Ni mshindi pia wa medali ya shaba katika michuano ya Olimpiki ya Rio 2016.

  • Boipelo Awuah, 15

    Afrika Kusini Ubao wa matairi

    Boipelo Awuah ni mwendeshasi wa kwanza wa ubao wa matiari kutoka Afrika Kusini kushiriki michuano ya Olimpiki. Pia, akiwa na miaka 15 ndiyo mwanamichezo mdogo zaidi kutoka Afrika katika michuano ya Tokyo 2020.

  • Blitzboks

    Afrika Kusini Raga ya wachezaji 7

    Timu ya Raga ya Afrika Kusini ya wachezaji 7 inayofahamika kama Blitzboks ilishinda medali ya shaba katika michuano ya Olimpiki ya Rio, 2016.

    Waliibuka washindi wa pili katika kombe la dunia la Raga ya wachezaji 7 mwaka 1997.

  • Oussama Mellouli, 37

    Tunisia Uogoleaji

    Ousama Mellouli ni mwogeleaji wa masafa marefu kutoka Tunisia ambaye alishinda medali ya dhahabu katika umbali wa mita 1500 katika Olimpiki ya Beijing 2008. Alishinda pia medali ya dhahabu katika marathoni ya kuogelea ya kilomita 10 katika michuano ya Olimpiki ya London 2012.

  • Marwa Amri, 32

    Tunisia Myeleka

    Marwa Amri ni mpigana myeleka kutoka Tunisia ambaye alishinda medali ya shaba katika michuano ya Olimpiki ya Rio 2016, na kuwa mwanamke wa kwanza kutoka Afrika kushinda medali ya myeleka katika michuano ya Olimpiki.

  • Ines Boubakri, 32

    Tunisia Fencing

    Ines Boubakri ni Mtunisia aliyeshinda medali ya shaba katika mchezo wa mapanga na kujjilinda wa fencing katika michuano ya Olimpiki ya Rio 2016.

  • Jacob Kiplimo, 20

    Uganda Mwanariadha

    Jacob Kiplima ni mkimbiajji wa mbio ndefu kutoka Uganda ambaye alishiriki mbio za mita 3,000 za IAAF ZA MWAKA 2020.

    Michuano ya Tokyo ya 2020 itakuwa ni Olimpiki yake ya pili.

  • Ronald Musagala, 28

    Uganda Mwanariadha

    Ronald Musagala ni mwanariadha wa Uganda alishiriki kwa mara ya kwanza Olimpiki Rio 2016 akikimbia mita 1,500.

    Alishinda medali za dhahabu katika Ligi ya Almasi ya mwaka 2019 katika miji ya London na Paris.

  • Joshua Cheptegei, 25

    Uganda Mwanariadha

    Joshua Cheptegei ni mkimbiaji wa mbio ndefu ambaye alishinda medali ya dhahabu katika mashindano ya wanaume ya dunia ya mwaka 2019 na kuandika rekodi mpya ya dunia ya mita 5,000 katika Ligi ya Almasi ya Monaco, mwaka 2020.

  • Peruth Chemutai, 22

    Uganda Mbio za viunzi

    Peruth Chemutai ni mkimbiaji wa kuruka viunzi kutoka Uganda. Alikamilisha mbio za wanawake za viunzi za mita 3,000 katika michuano ya Olimpiki ya Rio ya mwaka 2016.

    Alimaliza katika nafasi ya 5 mbio za wanawake za mita 3,000 katika mashindano ya dunia ya riadha ya mwaka 2019.

  • Copper Queens

    Zambia Kandanda

    Hii itakuwa michuano ya kwanza ya Olimpiki kwa timu ya taifa ya wanawake ya kandanda ya Zambia ama Copper Queens au She-Polopolo.

  • Scott Vincent, 29

    Zimbabwe Gofu

    Scott Vincent anashiriki kwa mara ya kwanza michuano ya Olimpiki. Mwaka 2019 alishika nafasi ya 4 katika michuano ya wazi ya Japani.

  • D'Tigers

    Nigeria Mpira wa kikapu

    Timu ya taifa ya kikapu ya wanaume ya Nigeria maarufu kwa jina la D'Tigers ndiyo timu pekee kutoka Afrika iliyofuzu moja kwa moja kushiriki michuano ya Olimpiki ya Tokyo 2020 kutokana na alama iliyozipata kupitia Kombe la Dunia la Kikapu, FIBA.

    Timu ya taifa ya kikapu ya wanaume ya Nigeria maarufu kwa jina la D'Tigers ndiyo timu pekee kutoka Afrika iliyofuzu moja kwa moja kushiriki michuano ya Olimpiki ya Tokyo 2020 kutokana na alama iliyozipata kupitia Kombe la Dunia la Kikapu, FIBA.

    Mabingwa hao wa Afrika pia wamezifunga timu za Australia na Marekani katika mechi za majaribio kujiandaa na Olimpiki mwezi Julai 2021.

  • The Pearls

    Angola Mpira wa Mikono

    Timu ya taifa ya wanawake ya mpira wa mikono ya Angola, maarufu kwa jina la The Pearls ndiyo mabingwa wa michuano ya Afrika ya 2021.

    Walishika nafasi ya nane katika michuano ya Olimpiki ya Rio mwaka 2016 baada ya kung'olewa katika hatua ya robo fainali.